Nchini Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo,matokeo ya uchaguzi mkuu wa Desemba 20, 2023 yamekataliwa na viongozi wa upinzani.
Watatu kati yao waliitisha maandamano leo, Moïse Katumbi, mgombea wa nafasi ya juu, Martin Fayulu aliyeshika nafasi ya tatu na Anzuluni Bembe anaendelea kusisitiza kuwa uchaguzi huo unafaa kubatilishwa na kurudiwa ili kurekebisha udanganyifu mkubwa.
Leo Rais Felix anaapishwa ikiwa ni mara ya pili, sherehe ya kuapishwa inafanyika katika uwanja wa Kinshasa. Kwa mara ya kwanza Laurent Désiré Kabila, aliapishwa kwenye uwanja huo tarehe 29 Mei 1997.