Rais wa Namibia Hage Geingob amefariki dunia wakati akipokea matibabu hospitalini katika mji mkuu, Windhoek.
Makamu wa rais Nangolo Mbumba ametangaza kuwa Geingob amefariki Leo alfajiri.
Kiongozi huyo mwenye umri wa miaka 82 aligunduliwa kuugua saratani na alitangaza hali yake mbele ya umma mwezi uliopita.