Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, TAMISEMI anayeshughulikia Afya, Dkt. Wilson Mahera amewataka waganga wafawidhi wa vituo vya kutolea huduma za afya ngazi ya msingi kuhakikisha wanawekeza katika mafunzo ili kuendana na mabadiliko ya teknolojia na kutoa huduma bora za afya kwa watanzania.
Ameyasema hayo wakati akifungua mkutano wa Waganga Wafawidhi wa vituo vya kutolea huduma za afya ngazi ya Msingi, Dkt. Mahera amesema waganga wafawidhi wanapaswa kuwekeza katika mafunzo kwa ajili ya maendeleo ya kitaalamu.