Mh. Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa Kassim amesema kuwa lengo la Serikali inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan ni kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora na za kisasa
![](https://www.togoromedia.co.tz/wp-content/uploads/2024/02/IMG_20240227_114808_289-1-1024x461.jpg)
Ameyasema hayo Leo wakati akizungumza na Wananchi Wilayani Butiama katika ziara yake mkoa wa Mara ambapo sambamba na hayo amesema kuwa vipaumbele vinavyohitaji utelelezaji wa haraka ni ujenzi wa stendi ya Magari na Soko la kisasa Wilayani Butiama
![](https://www.togoromedia.co.tz/wp-content/uploads/2024/02/IMG_20240227_111154_386-1-1024x535.webp)
Pia Waziri Mkuu ameongeza kwa kasema Serikali itajenga barabara za lami za mitaa pamoja na eneo la Mwitongo mahali yalipo makazi ya Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.