Rais wa awamu ya Pili wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ali Hassan Mwinyi amefariki Dunia leo jioni.
‘’Hayati mzee Ali Hassan Mwinyi, amekua akipatiwa matibabu tangu Novemba mwaka jana nchini Uingereza, na baadaye kurejea nchini alipokua akiendelea na matibabu katika hospitali ya Mzena, hadi umauti ulipomfika’’ Amesema Rais Samia.
Aidha Rais Samia ameongeza kuwa Tanzania itaombeleza kwa siku saba.
Rais Mwinyi anatarajiwa kuzikwa siku ya tarehe 2 machi huko visiwani Zanzibar.