Leo Machi 15, 2024 msanii wa Bongo flava nchini, Harmonize ametimiza umri wa miaka 30.
Katika ukurasa wake wa Instagram Harmonize ameandika… “Turn to 30 years of my life!! I just wanna thank everyone for supporting my music journey 8 years in the game and still number one, usitegemee kuniona nikifanya the same, nimechagua kuyakataa mabaya na kuyaendeleza mema. Naamini sikuzaliwa kuja kushindana wala kugombana!!!. Mapenzi ya watu wote yamefanya tuwe na Number One Record Label @Kondegang kama Yotube na mitandao mingine yote inavyo onyesha” – Harmonize
“Wakati huu moyo wangu umejawa na furaha sana najiona namuona KONDE BOY MPYA mwenye miaka (30) hagombani, hana kinyongo na yeyote, anayemtanguliza MUNGU.Nnimeona baadhi ya watu wakisema amani itapunguza utamu wa game. Mawazo yangu yanapingana na hilo maaana chuki zimekaa miaka kibao na hatujafikia kufanya makubwa wanayo fanya wenzetu Nigeria & South African, ifike mahala tuujaribishe upendo tuone nguvu yake”- ameongeza Harmonize.