Vifo vya wanafunzi vilivyotokana na ajali ya gari la Shule ya Msingi Ghati Memorial ya mkoani Arusha vimefikia vitano baada ya miili mimgine minne ya wanafunzi kupatikana.
Gari hilo lenye namba za usajili T 496 EFK lilianguka kwenye korongo mapema leo Aprili 12, 2024, ambapo mpaka sasa wanafunzi watatu, mwalimu na dereva wameokolewa wakiwa hai na zoezi la kutafuta miili mingine linaendelea.
Credit: IPP MEDIA