Ubalozi wa Norway Nchini, umesema utaendelea kushirikiana na Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine cha Morogoro – SUA, katika kufadhili na kutekeleza Miradi mbalimbali ya Kilimo, Ufugaji na mabadiliko ya Tabia ya nchi (Hewa ya ukaa).
Hayo yamebainishwa na Balozi wa Norway Nchini, Tone Tinnes katika ziara yake Chuoni hapo iliyolenga kutembelea na kukagua Miradi inayotekelezwa na SUA kwa kushirikiana na Norway.
Makamu Mkuu wa Chuo, Prof. Raphael Chibunda amesema ziara hiyo ni moja ya makubaliano ambayo SUA kilisaini na Chuo Kikuu cha Sanyansi Nchini Norway kufuatia ziara ya Rais Samia wamekubaliana kufanya mambo makuu matatu lakini kubwa zaidi ni kushirikiana katika sekta ya Kilimo.