Aliyekuwa Mtayarishaji wa Video za Muziki wa Bongo Flava Nchini, Khalfani Khalimandro amefariki Dunia
Director Khalfani alilazwa katika Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili (MOI) akiwa na tatizo la Damu kuvilia kwenye Ubongo lililomsababishia kupata Kiharusi (Stroke) upande wake wa kulia
Enzi za Uhai wake alijipatia umaarufu kwa kuongoza Video za Wasanii kama Aslay, Navy Kenzo, Christian Bella, Baby Madaha, Chinbees, Shilole na Linah.
Togoro Media inatoa pole kwa ndugu,jamaa na marafiki wote pamoja na Tasnia nzima ya burudani nchini.