Inakadiriwa kuwa idadi ya Camera za ulinzi (CCTV) 6,500 zenye mifumo ya Artificial Intelligence ( AI ) Technology zinatarajiwa kufungwa katika majiji makubwa manne hapa nchini.
![](https://www.togoromedia.co.tz/wp-content/uploads/2024/05/images-51.jpeg)
Mikoa ya Arusha, Dar Es Salaam, Dodoma na Mwanza ndio itakayonufaika na mradi huo ambao kwa mara ya kwanza unaanzishwa Tanzania na kwamba Camera hizo zitafungwa kwenye maeneo ya viwanda, maeneo ya biashara, sehemu za wazi zenye mikusanyiko, majiji, mitaa, hoteli na sehemu zenye huduma za kijamii.