Mbunge wa Jimbo la Tarime Vijijini, Mwita Waitara jana alikumbwa na wakati mgumu baada ya wananchi kumpokea kwa yowe, matusi na mabango ya kumkataa alipokwenda kushiriki mapokezi ya mwili wa kijana Justin Mataro (28) katani Sirari.
Kijana huyo alifariki dunia Juni 15, mwaka huu katika ajali ya gari iliyotokea katika Kata ya Itiryo na kujeruhi wengine 17 wakati wakitoka kwenye fainali ya mashindano ya Kombe la Waitara yaliyopewa jina la Waitara Cup.