Yanga SC imetangaza rasmi kuachana na Kiungo Mshambuliaji raia wa Ghana Augustine Okrah (30) baada ya kudumu na Yanga kwa miezi sita tu.
Augustine Okrah alijiunga na wana Jangwani hao January 2024 wakati wa Kombe la Mapinduzi ikiwa ni mara yake ya pili kucheza nchini baada ya mwaka 2022 kushindwa kufanya vizuri na Simba SC na kufungiwa virago.